Jinsi ya kupika Chapati za Maji

jinsi ya kupika chapati za maji


Jinsi ya kupika Chapati za maji: Leo ninakuletea hatua kwa hatua namna ya kuandaa na kupika Chapati laini. Tafadhali fuatana nami katika pishi hili.

Pishi: Chapati za maji/laini

Utangulizi: chapati laini ni kitafunwa au chakula kinachopendwa na na wengi. chakula hiki hupendwa zaidi na watu kwa sababu ni rahisi kutayarisha..

Mahitaji

  • Ngano 1/2 kilo
  • mayai 3
  • mafuta au samli 1/4 kikombe
  • kitunguu kikubwa kilichosagwa 1
  • Kitunguu Swaumu punje 4
  • Chumvi 1/2kijiko au kulingana na matakwa yako

Mahitaji

Namna ya kupika chapati za maji

  1. Chekecha unga wako vizuri weka katika bakuli safi.
  2. Tia maji katika bakuli la unga na ukoroge mpaka upate uji wa wastani si mzito san a wala si mwepesi sana.
  3. Ongeza mayai na chunmvi endelea kukoroga.
  4. Ongeza kitunguu swaumu na kitunguu maji. Injika kikaango chako jikoni subiri kipate moto.
  5. Chota pawa moja mimina na tandaza kuzunguka kikaango subiri sekunde tano hadi kumi mpaka ikauke kisha geuza upande wa pili.
  6. Tia mafuta huku ukigeuza na kuzungusha ili mafuta yaenee pande zote na ili chapati isiungue. Endelea kugeuza mpaka iwe rangi ya kahawia.
  7. Hapo chapati zitakua tayari kwa kuliwa.
  8. Fanya hivyo kwa chapati zote zilizobakia
Kiasi hichi kinatosha kupika chapati laini sita Mpaka kumi. Chapati za maji hupendeza zaidi kuliwa Michuzi mizito, Chai na kadhalika.