jinsi ya kuandaa Kachumbari mchanganyiko: Habari mpenzi wa blogu yetu, Leo tunakuletea namna ya kuandaa kachumbari mchanganyiko. Fuatana nami
Namna ya kuandaa kachumbari mchanganyiko hatua kwa hatua
Mahitaji muhimu
- Nyanya kubwa 2
- Vitunguu maji 3
- Karoti 3
- Pili pili hoho ya kijani 1
- pilipili hoho nyekundu 1
- Tango 1
- Kotmiri 1/2 fungu(1/2 kicha ) au 1/2 bunch
- Majani ya Iliki (parsley) 1/2 fungu (1/2 kichana) au 1/2 bunch
- Cerely vijiti 4
- Chumvi kiasi
- Ndimu kiasi
Jinsi ya kuandaa/kutayarisha
- Osha mbogamboga kwa kutumia maji safi ya uvugu vugu (pendelea kuosha saladi kwa kutumia maji ya namna hii ili kuua vijidudu)
- Katakata vitu vyote isipokuwa ndimu, kisha uweke katika mashine ya kusagia chakula (yaani food processor)
- Weka namba mbili kwenye mashine yako kisha Saga mchanganyiko wako kwa kusita sita kila baada ya sekunde 1 mpaka kachumbari yako ichanganyike vizuri.
- Ikishachanganyika vizuri, Weka maji ya ndimu kisha changanya na kijiko, Tia ndani ya bakuli tayari kwa kuliwa